Skip to main content

JINSI YA KUJA NA WAZO ZURI LA BIASHARA PART 1

 ๐Ÿ‘‰๐‘ฑ๐‘ฐ๐‘ต๐‘บ๐‘ฐ ๐’€๐‘จ ๐‘ฒ๐‘ผ๐‘ฑ๐‘จ ๐‘ต๐‘จ ๐‘พ๐‘จ๐’๐‘ถ ๐’๐‘ผ๐‘น๐‘ฐ ๐‘ณ๐‘จ ๐‘ฉ๐‘ฐ๐‘จ๐‘บ๐‘ฏ๐‘จ๐‘น๐‘จ. 


Ili kuweza kufanikiwa kwenye biashara unahitaji kuwa na wazo zuri la biashara. Je unajua jinsi ya kupata wazo hilo zuri la biashara? 


              ๐‘ท๐‘จ๐‘น๐‘ป 1

Watu wengi wamekuwa wakiniomba ushauri ni wazo gani zuri la biashara ambalo linaweza kuwapatia faida na mafanikio. Ukweli ni kwamba wazo ambalo ni bora kwa mtu fulani linaweza lisiwe bora kwako.


Moja ya sababu zinazofanya biashara nyingi kufa au kutokuendelea ni kuiga, yaani mtu akianza biashara leo baada ya muda unakuta watu wengine wameiga biashara ile ile, wanaifanya eneo lile lile na kwa mbinu zile zile. Hii ni njia rahisi sana ya kushindwa kwenye biashara.

Kuja na wazo la biashara kuna mambo mengi sana ya kuzingatia, hii ni pamoja na upo eneo gani, mkoa gani, elimu yako, watu waliokuzunguka, ujuzi, umri wako, muda, mtaji, resources, njaa yako, kiu ya kufanikiwa, connection, etc

Hivyo hakuna formula moja ambayo utatumia. Hapa chini nimejaribu tu kukupa njia mbali mbali kama muongozo. Unaweza chagua njia yoyote na kuanza nayo. 


     ๐Ÿ”นTUMIA UJUZI ULIO NAO

Ujuzi ulionao ndo sehemu ya kwanza kabisa ya kupata wazo la Biashara, Mfano kama wewe umejiriwa na ni fundi seremala, kwa nini usianze na wewe kuwa na biashara ya aina hiyo?


๐Ÿ”นBADILISHA HOBBY YAKO KUWA PESA

Hobby ni moja ya maeneo ambayo watu hupata mafanikio, kama wewe hobby yako ni Kuogelea, kwa nini usifundishe watu kuogelea?

Kuna njia mbali mbali unaweza tumia kuanzisha biashara kutokana na hobby yako pitia uzi huu



๐Ÿ”นNUNUA BIASHARA AMBAYO TAYARI IPO

Ukishindwa kabisa kupata wazo zuri unaweza nunua biashara ya mtu mwingine na kuindeleza, siku hizi kuna biashara kibao zinauzwa kwa sababu mbalimbali so unaweza nunua na kuendelea nayo. Kuna vigezo vya kuangalia kabla ya kununua.


๐Ÿ”นNINI KINAKOSEKANA MTAANI?

Tazama ni kitu gani hakipo hapo mtaani, geuza kuwa opportunity, inaweza isiwe ni mtaani ikawa ni kazini kwako, Kijijini kwenu au maeneo unayo kwenda kustarehe.

-Ni kitu gani huwa kinaleta usumbufu kwako na kukuchukulia muda mwingi na pesa nyingi?

-Ni huduma zipi hazipo kabisa mtaani kwako? Na ambazo ni za muhimu?

-Ni bidhaa zipi ambazo ni vigumu kuzipata mtaani kwenu?

-Ni kitu gani, wewe, Ndugu, Majirani huwa wanakilalamikia sana mtaani hapo?

-Ni tatizo gani sugu ambalo wewe mwenyewe hua linakusumbua na hujapata solution?

-Ni kitu gani umeona inaweza kua tatizo mbeleni? Mfano kwa sasa watu wanakula junk food bila kuangalia afya zao hili ni tatizo unaweza kuja na solution yake

-Huduma au bidhaa gani inaweza kuokoa pesa/muda wa mteja wako mtarajiwa?

-Huduma gani inaweza rahisisha maisha ya mtu?


๐Ÿ”นANGALIA MAKAMPUNI MAKUBWA WANAHITAJI NINI?

Unaweza tumia uwepo wa makampuni Fulani au taasisi Fulani maeneo yako kutengeneza wazo la biashara, taasisi kama Shule, vyuo, Hospitali, Makampuni kama Viwanda Migodi na kadhalika, angalia ni kipi hawa watu wanaweza kuwa wanahitaji.


๐Ÿ”นUNAWEZA KUANGALIA KUHUSU KUUZA BIDHAA ZA WENGINE

Unaweza ukawa unauza bidhaa za watu wengine, unachukua na kuuza. Fanya utafiti kabla ya kuanza kuuza bidhaa hizi. Mfano miezi miwili mitatu nyuma kuna mafuta ya wanawake yanaitwa Snail yameuzwa sana. Hii ilikua bidhaa nzuri


๐Ÿ”นANGALIA HABARI NA MAKALA MBALIMBALI

Kuna chaneli huwa zina makala mazuri sana ya kiuchumi na biashara, kitaifa na kimataifa siku huzi kazi yao ni hiyo tu, ni kuonyesja ubunifu wa wajasirimali, TV, radio na magazeti yanaweza toa mchango wakutosha kwa wewe kupata wazo la biashara


๐Ÿ”นCOPY BUSINESS IDEA AMBAYO IMEFANIKIWA KWINGINEKO

Hii ni moja ya njia zinazo tumika kwa sasa, unaweza copy idea kutoka hata India, China, na kwingineko na ukaja kuifanyia kazi huku kwa kufanya marekebisho madogo kulingana na mahitaji ya eneo husika


๐Ÿ”นTUMIA NJIA ZOTE ZA KIUTAFITI KUPATA WAZO LA BIASHARA

- Maonyesho ya biashara

- Kwenye taasisi za uma zinazo husika na biashara

- Kwa marafiki.


๐Ÿ”นMITANDAO YA KIJAMII

Watu kwenye mitandao ya kijamii ni rahisi sana kupost kuhusu matatizo na kero zao kuhusu huduma au bidhaa flani. Wachache hua wanafuatilia na kutatua matatizo hayo. Matatizo hayo yanaweza kua chanzo cha wazo bora la biashara.


๐Ÿ”นWEBSITE ZA BIASHARA

Kuna kurasa za Instagram ambazo hua wanauza vitu mbali mbali au mitandao kama ebay, AliExpress, AliBaba, Kikuu, Inalipa, etc pendelea kuitembelea na kuangalia bidhaa zinazouzwa humo ni chanzo kizuri cha mawazo ya biashara


๐Ÿ”นTEMBELEA MASOKO MAKUBWA

Kwa kutembelea masoko makubwa kama Kariakoo na mengine kama hayo. Yanaweza kukufungua akili kufahamu biashara gani ya kufanya. Kwa kuangalia bidhaa aina gani zinatoka au wateja wanazikimbilia.


๐Ÿ”นUNAWEZA GUNDUA KITU?

Unaweza ukaja na ugunduzi wako kama kuna jamaa nilimuona TBC katengeneza mashine zake za kukunia nazi kwa umeme. Jamaa anauza mashine 300,000 mashine hizo nikakuta kariakoo vijana wanatumia kukunia nazi moja 200. Kwa siku jamaa wanakuna nazi hadi 500

Kama tulivyoona hapo juu hizo ni baadhi tu ya njia unazoweza kuzifanya ukiwa unatafuta wazo la biashra. Kama kunayoyote nimeisahau unawea kuiongezea.


๐™„๐™‰๐˜ผ๐™€๐™‰๐˜ฟ๐™€๐™‡๐™€๐˜ผ ๐™‹๐˜ผ๐™๐™ 2.........

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAJI ( MULTI PURPOSE LIQUID SOAP)

*๐Ÿ›‘VIFAA MAMA KTK SABUNI YA MAJI*๐Ÿ‘‡๐Ÿปni hivi ndio vinafanya iitwe  sabuni ๐Ÿ‘‡๐Ÿป *Sulphonic acid* *Sless* *Rangi* *Chumvi.* *Manukato* *๐Ÿ‘‰Sulphonic acid* kazi yake kubwa ni kuondoa uchafu wa mahali wakati unatumia sabuni, pia inaongeza uzito na povu ktk sabuni yetu, sulphonic acid ikizidishwa ktk sabuni huleta mchubuko wa mikono kea mtumiaji. *๐Ÿ‘‰Manukato-* kwaajili ya harufu. *๐Ÿ‘‰Sless( ungarol)* Kai yake ni kuleta povu, kuongeza uzito, na pia huondoa uchafu wa mahali wakati unapotumia sabuni. *๐Ÿ‘‰Rangi* Kuleta rangi ya sabuni pekee. *๐Ÿ‘‰Chumvi* Huongeza uzito ktk sabuni, hutunza sabuni isiharibike, pia ikizidishwa hukata sabuni na kuifanya iwe nyepesi Kama maji na kuisha povu. *๐Ÿ›‘Hivi ndio๐Ÿ‘†๐Ÿฝ vifaa mama ktk utengenezaji was sabuni ya maji* *๐Ÿ›‘Vifaa vya nyongeza๐Ÿ‘‡๐Ÿป* *๐Ÿ“š Gryselin-* kazi yake kubwa ni kulainisha sabuni na kuzuia michubuko ya ngozi kwa mtumiaji wa sabuni hiyo. *๐Ÿ“š Formaline-* kazi ya yake kutunza sabuni isiharibike, ila formaline ...

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI Biashara ya kuuza Rasta na Mawigi kwa bei ya jumla, wengi wanapata shida kuja paka Dar kununua Rasta na Mawigi kwa gharama ya juu, mfanyabiashara akiwa mgeni Dar anatumia gharama kubwa sana kwa kufikia Guest pamoja na Chakula. Kama ukiwai kutoa hii huduma kwa wafanyabiashara wa mikoani ni FURSA kwako na unakuwa umewasaidia kupunguza gharama kubwa na kupata faida kuwa kwao. Ukitaka kufanikiwa katika hii biashara fanya yafuatayo : Tafuta maduka yanayouza RASTA & MAWIGI kwa bei ya chini. Ili uweze kutoa OFA nzuri na kupata wateja wengi wa mikoani na kuwasaidia nao kupata faida kubwa kwa kununua kwako. Fungua Instagram Account; post RASTA & MAWIGI aina mbalimbali na bei zake, kumpa mteja njia nyingi za kuchagua bidhaa anayotaka kwenda kuuza kwa wateja wake. Pia post video za watu waliosuka kwa kutumia bidhaa zako au waliotumia kwa kupiga picha. Tumia Bank Account, kupokea malipo kutoka kwa wateja wako; kwa kutumia bank akaunti utakuwa umejilind...

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAGADI/KIGOMA/GWANJI

Jinsi ya kutengeneza Sabuni ya magadi( gwanji)ama Sabuni ya kigoma. MAHITAJI Caustic Soda kilo 3 Mafuta ya mawese lita 20 Sodium Silicate Maji lita 10 Rangi ya bluu vijiko 3 Jinsi ya kutengeneza. 1)Chukuwa coustic soda changanya na maji na uanze kukoroga kuelekea upande mmoja endelea kufanya hivyo hadi vichanganyikane vizur baada ya hapo iache kwa saa 24 2)Chukuwa kindoo kidogo na upunguze mafuta lita 3 kwa ajili ya kuweka rangi pembeni,weka rangi vijiko 3 ,changanya na mafuta uliyopunguza lita 3 kisha koroga mpaka yachanganyikane vizur kabisa 3)Chukuwa coustic soda uliyoloweka kwenye ndoo kubwa ,kisha tia mafuta na uendelee kukoroga kuekekea upande mmoja kwa nguvu na kwa haraka,tia sodium silgett kwa kunyunyuzia kidogo kidogo, endelea kukoroga hadi vichanganyikane viwe kitu kimoja 4)Baada ya hapo andaa ndoo nyingine ndogo ,chukuwa uji uliokoroga au mkorogo wako kias kwa ajili ya kuchanganya na rangi mwanzo na mafuta kisha koroga kwa pamoja vichanganyikane vizur ...