Skip to main content

JUICE YA MAGANDA YA NANASI


 ▶FAIDA ZA JUICE YA MAGANDA YA NANASI NA JINSI YA KUIANDAA KAMA TIBA.

_____________________________

NANASI ni tunda lenye ladha nzuri. Mbali na kutumika kama tunda ama juisi yake kutumika kama kinywaji, tunda la nanasi lina faida mbalimbali kwa afya ya mwanadamu.


Baadhi ya faida hizo ni pamoja na :

____________________________


i. UTAJIRI WA VITAMINI NA MADINI :

Nanasi ina vitamini A,B na C na pia ina madini ya chuma, calcium, copper na phosphorous ambayo yote ni muhimu sana katika afya ya mwanadamu.


ii. Tunda hili husaidia kutengeneza damu


iii. Nanasi husaidia kuimarisha mifupa , meno, neva na misuli (muscles).


iv. Tunda la nanasi hutibu matatizo ya tumbo.


v. Hutibu matatizo ya Bandama


vi. Hutibu matatizo ya Ini


vii. Husaidia kusafisha Utumbo mwembamba


viii. Husaidia kutibu Homa


ix. Husaidia kutibu Vidonda mdomoni


x. Husaidia kutibu Magonjwa ya koo


xi. Husaidia kutibu tatizo la Kupoteza kumbukumbu


xii. Husaidia kutibu maradhi ya akili Kukosa mori (low spirit)


xiii. Husaidia kutibu Kikohozi


xiv. Husaidia kutibu tatizo la Kutetemeka


xv. Husaidia kutibu tatizo la Woga ( Anxiety )


xvi. Husaidia kutibu matatizo ya wanawake (upungufu wa hormones au makosa fulani katika sehemu za siri )


xvii. Huondoa shida ya kufunga choo


xviii. Hutibu tatizo la baridi yabisi


xix. Husaidia katika kutibu tatizo la Upungufu wa damu


xx. Pia tunda hili huwasaidia akina mama wanaonyonyesha (uhaba wa maziwa)


▶Jinsi yakutengeneza juisi itokanayo na maganda ya nanasi

_____________________________


```1.Lisafishe nanasi kwa maji safi```


```2.Chonga nanasi lako vizuri kama unavyochonga nanasi la kukata vipande vya matunda, ila wakati huu ukihifadhi maganda yake kwenye chombo safi kama vile sinia, badala ya kuyatupa kwenye ndoo ya uchafu.```


3.Yaweke maganda ya nanasi kwenye sufuria au chungu cha kuchemshia


4.Tia maji ya kutosha kufunika maganda ya mananasi


5.Injika sufuria/chungu jikoni katika moto wa wastani ili ipate moto na kukaribia kuchemsha.


6.Punde tu yanapokuwa yamepata joto la kutosha na kukaribia kuchemka, epua sufuria/chungu toka jikoni.


7.Acha chombo hicho kilivyo na kifunike vizuri kiendelee kupoa, unaweza kuacha hata kwa saa 12 hadi 24 kulingana na hali ya hewa (ukizingatia sana kwenye maeneo ya joto kutokuacha muda mrefu ili isichachuke).


8.Chukua chombo na mimina kwa kuchuja ili kutenganisha juisi na maganda.


9.Gawa juisi kama kinywaji, waweza kuweka barafu kuongeza baridi kadiri ya upendeleo wa mnywaji vile vile unaweza kuongeza asali au sukari kuongeza ladha kadiri ya mtumiaji atakavyo!

                   

ZIADA:

Unaweza kuweka sukari/asali kabla ya kuinjika sufuria/chungu jikoni.

Unaweza kuongeza mdalasini, Iliki au Karafuu kulingana na uhitaji wako. Ni nzuri sana kuandaa juisi kama unajali na unaipenda familia yako. Kuliko kuwanunulia soda za takeaway wanunulie nanasi wajenge afya zao.


Kama umependa weka comment yako  hapo chini.  

                      0748491485

                    nyamka_enterpises

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAJI ( MULTI PURPOSE LIQUID SOAP)

*🛑VIFAA MAMA KTK SABUNI YA MAJI*👇🏻ni hivi ndio vinafanya iitwe  sabuni 👇🏻 *Sulphonic acid* *Sless* *Rangi* *Chumvi.* *Manukato* *👉Sulphonic acid* kazi yake kubwa ni kuondoa uchafu wa mahali wakati unatumia sabuni, pia inaongeza uzito na povu ktk sabuni yetu, sulphonic acid ikizidishwa ktk sabuni huleta mchubuko wa mikono kea mtumiaji. *👉Manukato-* kwaajili ya harufu. *👉Sless( ungarol)* Kai yake ni kuleta povu, kuongeza uzito, na pia huondoa uchafu wa mahali wakati unapotumia sabuni. *👉Rangi* Kuleta rangi ya sabuni pekee. *👉Chumvi* Huongeza uzito ktk sabuni, hutunza sabuni isiharibike, pia ikizidishwa hukata sabuni na kuifanya iwe nyepesi Kama maji na kuisha povu. *🛑Hivi ndio👆🏽 vifaa mama ktk utengenezaji was sabuni ya maji* *🛑Vifaa vya nyongeza👇🏻* *📚 Gryselin-* kazi yake kubwa ni kulainisha sabuni na kuzuia michubuko ya ngozi kwa mtumiaji wa sabuni hiyo. *📚 Formaline-* kazi ya yake kutunza sabuni isiharibike, ila formaline ...

JINSI YA KUTENGENEZA HAIR SHAMPOO

 ▶ HAIR SHAMPOO◀ _______________________ Hii ni sabuni ambayo imebuniwa kwa ajili ya kusafishia nywele hata kama zimekaa muda mrefu bila kusafishwa. Hufanya nywele ziwe safi, huondoa uchafu na kuua wadudu walioko kwenye nywele na huondoa mba kwenye nywele. Hapa tutajifunza aina tofauti tofauti za shampoo zikiwemo zenye virutubisho vya matunda na mimea. ▶ SHAMPOO YA NYWELE NZITO NA BORA. 👉MALIGHAFI. 🔸Sless – 1kg. 🔸Cde – 250gm. 🔸Gryceline – vijiko vitano vya chakula (50ml). 🔸Chumvi -500gm. 🔸Rangi – 5gm. 🔸Perfume – 5gm. 🔸Formaline /citric acid – vijiko 3. 🔸Tigna – 125gm. 🔸Maji – 25lt. 👉VIFAA. 🔹Mwiko. 🔹Beseni. 🔹Mask. 🔹Miwani. 🔹Koti. ▶JINSI YA KIUTENGENEZA◀ 1⃣Andaa maji lita 12 kisha tia humo tigna na koroga hadi upate uji mzito kisha weka kando. 2⃣Chukua sless koroga ndani ya maji lita 12 hadi iyeyuke kabisa kisha weka kando. 3⃣Chukua maji nusu lita korogea humo chumvi 500gm hadi iyeyuke yote kisha weka kando.  4⃣Chukua maji robo lita  tia  rangi na korog...

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI Biashara ya kuuza Rasta na Mawigi kwa bei ya jumla, wengi wanapata shida kuja paka Dar kununua Rasta na Mawigi kwa gharama ya juu, mfanyabiashara akiwa mgeni Dar anatumia gharama kubwa sana kwa kufikia Guest pamoja na Chakula. Kama ukiwai kutoa hii huduma kwa wafanyabiashara wa mikoani ni FURSA kwako na unakuwa umewasaidia kupunguza gharama kubwa na kupata faida kuwa kwao. Ukitaka kufanikiwa katika hii biashara fanya yafuatayo : Tafuta maduka yanayouza RASTA & MAWIGI kwa bei ya chini. Ili uweze kutoa OFA nzuri na kupata wateja wengi wa mikoani na kuwasaidia nao kupata faida kubwa kwa kununua kwako. Fungua Instagram Account; post RASTA & MAWIGI aina mbalimbali na bei zake, kumpa mteja njia nyingi za kuchagua bidhaa anayotaka kwenda kuuza kwa wateja wake. Pia post video za watu waliosuka kwa kutumia bidhaa zako au waliotumia kwa kupiga picha. Tumia Bank Account, kupokea malipo kutoka kwa wateja wako; kwa kutumia bank akaunti utakuwa umejilind...