Skip to main content

TABIA YA MTU MWENYE NAFASI KUBWA YA KUFIKIA NDOTO YAKE

TABIA YA MTU MWENYE NAFASI KUBWA YA KUFIKIA NDOTO YAKE
____

๐Ÿ”† *Mtu anayemcha na kumtegemea mungu*

 Utajiri na heshima ziko kwangu, Naam, utajiri udumuo, na haki pia. ~Biblia

Kuna watu huwa wana kawaida ya kutenganisha mafanikio na Mungu,watu hawa ni wale wanaotaka vitu kwa njia za mkato . Hawa ndio wale wanajiunga na vyama vya kishetani huku wakisahau kuwa hata shetani alikuwa wa Mungu na baadae akaasi. Mtu mwenye utajiri wa kishetani huwa haudumu.

 Mafanikio ya kweli yanatoka kwa Mungu kinyume na hapo twajidanganya wenyewe .Sisi wote tulitokana na Mungu na yeye ndiye aijuaye kesho yetu. Ukweli tunajitahidi kupanga mengi lakini Mungu asipoingilia hakuna matokeo yoyote (Bwana asipoijenga nyumba waijengao wafanya kazi bure. Bwana asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha bure~Biblia)

๐Ÿ”† *Mtu anayejaribu vitu*

Mtu anayejaribu vitu vingi huyu siku moja atafanikiwa .Haikuwa rahisi kwa Thomas Edson kufiki ndoto yake mpaka alipojaribu mara 1000 , lakini mwisho wa siku akafanikisha .Leo tunafurahia matokeo mazuri ya majaribio ya Edson. Ukweli ni kwama mtu anayejaribu vitu lazima atafanikiwa, hukumbuki hata huyo ndugu/rafiki/jirani  yako alivyokuwa ni mtu wa kujaribu vitu na sasa amefanikiwa? Anza kuwa mtu wa kujaribu vitu haijalishi unashindwa mara ngapi.

๐Ÿ”† *Mtu mwenye bidii*

Mtu mwenye bidii mafanikio kwake ni lazima lakini mtu mvivu ajiandae kuajiriwa na mtu mwenye bidii kwa sababu watu wanaopenda kuajiriwa(kutimiza ndoto za wengine) miaka yote ni watu wavivu wasiopenda kuumiza akili,mwili n.k. Kama wewe una bidii mafanikio yako lazima cha msingi endelea kufanya kwa bidii bila kuchoka. Fanya kila kitu kwa bidii kubwa haijalishi huoni matokeo haraka.

๐Ÿ”† *Mtu mwenye maarifa*

Maarifa aliyonayo mtu ndiyo humsaidia kugundua fursa ambazo watu wengine hawazioni ambazo ndizo zinamfanikisha mtu. Kwani mchezaji anayefunga sana magoli hata kama beki ya wapinzani wake iko imara siri yake ni nini? Siyo uchawi lakini ni kwa sababu maarifa yake yako juu ya mabeki na kwa hiyo hawezi kuzuulika ndivyo ilivyo kwa mtu mwenye maarifa hawezi kuzuilika kutimiza ndoto zake maana anajua namna ya kupenya hata mahali ambapo inaonekana hapana njia ya kupita kabisa.

๐Ÿ”† *Mtu asiyekata tamaa*
 Mtu asiyekata tamaa lazima atafanikiwa maana kila siku atakuwa anatafuta mpenyo wa kufikia ndoto yake. Hapa ndipo watu wengi wanashindwa na ndiyo maana wengi wanakufa na ndoto zao. Naelewa njiani kuna magumu mengi lakini wale wanaovumilia mpaka mwisho ndio pekee hufanikiwa.


๐Ÿ”† *Mtu anayesimamia kile anachokiamini*

Rafiki yangu Mwalimu Robison Sisyan  mwandishi  wa makala za kibiashara  wakati fulani akiwa anafundisha kwenye kundi moja la WhatsApp alisema  ili uweze kufanikiwa ni lazima kwanza uwe na uwezo wa kusimamia kile unachokiamini pale ambapo watu wanaweza kukukosoa kwa kuonesha ni namna gani huwezi kufanikiwa."

Huwa iko hivi na kila siku itakuwa hivyo kwamba watu wanaoamini mawazo yao na kuyasimamia ndio wanaofanikiwa bila kukatishwa tamaa wakiamini kuwa siku moja watakuja kufanikiwa kinyume na hapo kama ni mtu wa kusiliza watu wanaokuvunja moyo utakuwa unatwanga maji kwenye kinu,hutafika kokote.

๐Ÿ”† *Mtu mwenye mahusiano mazuri na watu*

Mahusiano mazuri na watu  ndiyo huleta mafanikio haraka. Mtu mwenye mahusiano mazuri na watu atakuwa na fursa nyingi ambazo zingine huzipata kutokana na mahusiano mazuri aliyojenga. Mtu huyu ni rahisi kusaidiwa pale anapohisi kushindwa. Mtu mwenye mahusiano mabaya na watu si rahisi kufikia kwenye ndoto na mafanikio anayoyataka.

๐Ÿ”† *Mtu anayejua thamani ya muda*

Mafanikio yako katika muda.Kwa bahati mbaya watu wengi huwa wanatumia muda ovyo ovyo huku wakishau kuwa muda ni mali haupaswi kuchezewa. Watu waliofanikiwa ni watu walio makini sana na matumizi ya muda .Wanajua  kuwa muda hauwezi kujirudia katika maisha kwa maana hiyo wanakuwa makini sana na matumizi ya muda.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAJI ( MULTI PURPOSE LIQUID SOAP)

*๐Ÿ›‘VIFAA MAMA KTK SABUNI YA MAJI*๐Ÿ‘‡๐Ÿปni hivi ndio vinafanya iitwe  sabuni ๐Ÿ‘‡๐Ÿป *Sulphonic acid* *Sless* *Rangi* *Chumvi.* *Manukato* *๐Ÿ‘‰Sulphonic acid* kazi yake kubwa ni kuondoa uchafu wa mahali wakati unatumia sabuni, pia inaongeza uzito na povu ktk sabuni yetu, sulphonic acid ikizidishwa ktk sabuni huleta mchubuko wa mikono kea mtumiaji. *๐Ÿ‘‰Manukato-* kwaajili ya harufu. *๐Ÿ‘‰Sless( ungarol)* Kai yake ni kuleta povu, kuongeza uzito, na pia huondoa uchafu wa mahali wakati unapotumia sabuni. *๐Ÿ‘‰Rangi* Kuleta rangi ya sabuni pekee. *๐Ÿ‘‰Chumvi* Huongeza uzito ktk sabuni, hutunza sabuni isiharibike, pia ikizidishwa hukata sabuni na kuifanya iwe nyepesi Kama maji na kuisha povu. *๐Ÿ›‘Hivi ndio๐Ÿ‘†๐Ÿฝ vifaa mama ktk utengenezaji was sabuni ya maji* *๐Ÿ›‘Vifaa vya nyongeza๐Ÿ‘‡๐Ÿป* *๐Ÿ“š Gryselin-* kazi yake kubwa ni kulainisha sabuni na kuzuia michubuko ya ngozi kwa mtumiaji wa sabuni hiyo. *๐Ÿ“š Formaline-* kazi ya yake kutunza sabuni isiharibike, ila formaline ...

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI Biashara ya kuuza Rasta na Mawigi kwa bei ya jumla, wengi wanapata shida kuja paka Dar kununua Rasta na Mawigi kwa gharama ya juu, mfanyabiashara akiwa mgeni Dar anatumia gharama kubwa sana kwa kufikia Guest pamoja na Chakula. Kama ukiwai kutoa hii huduma kwa wafanyabiashara wa mikoani ni FURSA kwako na unakuwa umewasaidia kupunguza gharama kubwa na kupata faida kuwa kwao. Ukitaka kufanikiwa katika hii biashara fanya yafuatayo : Tafuta maduka yanayouza RASTA & MAWIGI kwa bei ya chini. Ili uweze kutoa OFA nzuri na kupata wateja wengi wa mikoani na kuwasaidia nao kupata faida kubwa kwa kununua kwako. Fungua Instagram Account; post RASTA & MAWIGI aina mbalimbali na bei zake, kumpa mteja njia nyingi za kuchagua bidhaa anayotaka kwenda kuuza kwa wateja wake. Pia post video za watu waliosuka kwa kutumia bidhaa zako au waliotumia kwa kupiga picha. Tumia Bank Account, kupokea malipo kutoka kwa wateja wako; kwa kutumia bank akaunti utakuwa umejilind...

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAGADI/KIGOMA/GWANJI

Jinsi ya kutengeneza Sabuni ya magadi( gwanji)ama Sabuni ya kigoma. MAHITAJI Caustic Soda kilo 3 Mafuta ya mawese lita 20 Sodium Silicate Maji lita 10 Rangi ya bluu vijiko 3 Jinsi ya kutengeneza. 1)Chukuwa coustic soda changanya na maji na uanze kukoroga kuelekea upande mmoja endelea kufanya hivyo hadi vichanganyikane vizur baada ya hapo iache kwa saa 24 2)Chukuwa kindoo kidogo na upunguze mafuta lita 3 kwa ajili ya kuweka rangi pembeni,weka rangi vijiko 3 ,changanya na mafuta uliyopunguza lita 3 kisha koroga mpaka yachanganyikane vizur kabisa 3)Chukuwa coustic soda uliyoloweka kwenye ndoo kubwa ,kisha tia mafuta na uendelee kukoroga kuekekea upande mmoja kwa nguvu na kwa haraka,tia sodium silgett kwa kunyunyuzia kidogo kidogo, endelea kukoroga hadi vichanganyikane viwe kitu kimoja 4)Baada ya hapo andaa ndoo nyingine ndogo ,chukuwa uji uliokoroga au mkorogo wako kias kwa ajili ya kuchanganya na rangi mwanzo na mafuta kisha koroga kwa pamoja vichanganyikane vizur ...