Skip to main content

FURSA ZA MTAJI WA LAKI MOJA KWA WAJASIRIAMALI WADOGO


Fursa za mtaji wa laki moja (100,000) kwa wajasiriamali wadogo

Laki moja naweza kufanyia biashara gani?

Fursa za laki ni nyingi sana kwa alieamua kutoka ndani na kuingia mtaani. Kabla hujaendelea naomba nikupe angalizo.



Kama hujaamua kutoka ndani na kuingia mtaani ama kwa lugha nyengine kama hujaamua kufuta aibu kichwani mwako basi hii makala haikufai.



Fursa hizo ni kama:-



MAMA NTILIE, KIJIWE CHA CHIPS, KIJIWE CHA SUPU, KIJIWE CHA NYAMA CHOMA & MISHKAKI, KIJIWE CHA PWEZA, KIJIWE CHA MATUNDA (MATIKITI YA KUCHONGA), ETC



Kwa kawaida kila penye watu wengi ambao huwepo kwa muda mrefu basi pana wateja wa aina 2. Wa kipato kikubwa na kidogo.



Maeneo mengi yenye watu wengi panakuwa na migahawa kadhaa. Mathalan kwenye mahospitali makubwa kama muhimbili, kwenye vituo vikubwa vya mabasi kama ubungo, kwenye viwanja vikubwa kama taifa, etc.



Humu kote kuna migahawa. Unachopaswa kufanya ni kuangalia je hisi sehemu zinapatikana milo ya kimaskini? Assume mtu ana nja na bajeti yake ni 1000 tu je unaweza kumuuzia chakula kwa bei hiyo?



Wengi wa hawa wa bajeti za chini wanachoangalia zaidi ni chakula kisafi cha kushiba. Hawana mbwembwe ya mboga mbili tatu. Hata kama ni wali maharage ni sawa tu ilimradi iwe katika bajeti yake.



Makala hii itaendelea. Tutapitia fursa nyingi sana za mtaji wa laki moja. Usikose kuendelea kufuatilia ukurasa huu.



Nini cha kufanya kama una mtaji zaidi ya laki

NINI CHA KUFANYA KWA WENYE MITAJI MIKUBWA?



Kabla ya kuendelea na zile fursa za biashara za laki moja nimeona nitoe angalizo kwa wale wenye mitaji mikubwa kiasi.



Ukiwa na mtaji mkubwa kiasi haina maana kuwa ndio ujiingize katik idea kubwa kubwa. Bali ingia kwenye idea ndogo ndogo na uzifanye kwa ukubwa.



FAIDA YAKE

Faida ya huu mtindo ni kwamba unaweza kuisoma biashara na kuiteka gafla. Mfano ni mtindo anaoutumia Bakresa kuzichukua idea ndogo na kuzifanya kwa ukubwa.



Tumeona ice cream, tumeona juice, tumeona ukwaju, tumeona karanga, tumeona ubuyu, na kadhalika na kadhalika.



MFANO

Labda wewe una milioni kumi ama zaidi na unawaza biashara ya kufanya. Unaweza ukachukua idea hizi za laki ukazifanya kwa ukubwa zaidi kama anavyofanya Bakresa.



Tuchukulie umeamua kuifanya ile ya mayai. Utakachokifanya ni kuifanya kwa kiwango cha kisasa na kikubwa.



Wale vijana kwako watakuwa mawakala. Mtaingia mikataba. Utawapa tisheti. Utawapa kiwango wanachotakiwa kuuza kwa siku. Utawapa mafunzo ya ujasiriamali na utawalipa commission. Watauza kama wale wa Baressa wanavyouza ukwaju.



Inatakiwa pia kujenga brand mitandaoni. Hakikisha unakuwa na posts nyingi sana zinazoongelea biashara hii. Usione hasara kuwa na camera man wako maalum kwa siku awe anapiga picha za kutosha na ku edit.



ANGALIZO

Biashara ndogo ni nyepesi wengine kuiga hivyo unatakiwa kuwa na ubunifu wa ziada. Kila mara kaa na watu unaoamini kuwa wana ubunifu na wakupe maoni yao.



Bahati mbaya sana watanzania tukishasimama katika biashara tuna ignore kutafuta ushauri mpaka tuanguke.



Ukiwa karibu na wabunifu ni rahisi kutumia hili gurudumu kupanua wigo wako kila mara kuliko kusubiri wengine waige na kuanza kulalama.



Fursa namba moja ya mtaji wa laki moja

Mradi wa kwanza wa laki moja ambao nitauzungumzia ni wa biashara ya mayai ya kuchemsha. Mradi huu utakuhitaji kuajiri kina/binti mmoja au zaidi kulingana na upatikanaji na uaminifu wa vijana ambao unahisi watakufaa.



Katika mfano wangu ambao nitatumia eneo la dar:



 Nita ajiri vijana watatu ambao nawafahamu mwenendo wao.

 Nitanunua mayai trey 9 pamoja na trey zake. Hapa nitatumia kati ya 70,000 hadi 90,000.

 Nitanunua chumvi pakti moja.

Nitachemsha hayo mayai trey zote 9.

 Kila kijana ataondoka na trey tatu asubui na kwenda kuuza maeneo ya mchanganyiko ikiwa either ni stendi na sehemu kama hizo.

Makubaliano kwa vijana hao watatu ni kwamba kila trey ambayo mtu anauza nitamlipa shilingi 3000. Na bei ya yai wanapaswa wauze shilingi 500.

Mapato kwa siku ya kwanza yatakuwa 500x30x9 = 135,000. Kati ya hizo nitawapa vijana shilingi 9,000 kila mmoja.

Ratiba itaendelea hivyo kwa muda na nitapanua biashara itakapobidi.

Gharama zingine ndogo ndogo ni kama mkaa na chumvi na ni kiasi kidogo sana.



Hivyo gharama zetu ni:

Mayai na trey zake = maximum 90,000

Malipo kwa vijana = 27,000

Chumvi, mkaa = 3,000



Jumla 120,000.



Mauzo 135,000 toa gharama 120,000 sawa na faida 15,000. Kuanzia siku ya pili faida itaongezeka mana hatununui mayai na trey zake bali tunanunua mayai pekee.







Fursa namba mbili ya mtaji wa laki

Fursa ya pili ya laki moja ambayo nitaizungumzia ni biashara ya genge. Genge ni sehemu muhimu sana katika maisha ya mitaani. Wachache sana huku mitaani kwetu ambao huenda shopping ya kujaza vitu ndani.



Wengi wetu hununua mahitaji ya papo kwa papo. Hebu toka tembea tembea na uangazie mazingira ya mitaani kwenu, mitaa ya jirani, mitaa ya mbali kidogo, mitaa ya sokoni, etc.



Katika tembea tembea yako angalia ni wapi pana uhaba wa magenge. Na pia unapopita magengeni angalia viashiria vya soko kuwepo. Ukipita sehemu ukaona watu husubiria kuhudumiwa mmoja mmoja na wapo wengi jua kuwa hapo kuna fursa kubwa sana.



Pachunguze na uorodheshe mambo ambayo kwako unaona ni mapungufu ya hilo au hayo magenge. Ukishaorodhesha mapungufu angalia na ubuni njia ya kuwa na genge ambalo litatoa nafuu kwa wateja.



VITU VYA MSINGI GENGENI



Mboga majani

 Vingia mchuzi kama nyanya, carrots, hoho, vitunguu, etc

Viungo vya ziada kama iliki, dalasini, swaumu, etc

Matunda kama tikiti, tango, chungwa, papai, parachichi, embe, nanasi, etc

Viazi, nazi, ndizi mbichi, etc

NJIA ZA KUJUA FAIDA

Kupata urahisi orodhesha hivi vitu katika karatasi ya shopping na uweke idadi. Ukimaliza pita magenge kadhaa na ukifika uliza bei ya vitu hivyo na uinakili.



Ukimaliza nenda sokoni wanapouza bidhaa hizo bei za jumla. Uliza bei na uorodheshe bei hizo.



Fanya hesabu katika laki moja utaanza na idadi gani ya vitu gani mana hutomudu kuweka kila kitu kwa laki moja ila pia hutokosa soko hata kama utakuwa na vitu vya elfu 20.



Ukishamaliza hesabu za hapo juu linganisha jumla ya pesa utayotumia ukinunua vitu hivyo kwa bei ulizoona sokoni na jumla ya mapato utayoyapata ukiuza bidhaa hizo. Tofauti yake huwa ni faida yako.



KWA MFANO

Kwa kawaida sado moja ya viazi utauziwa kati ya 3,000 hadi 4,500 kulingana na sehemu. Tathmini kadhaa zilizofanyika zinaonesha kuwa sado moja huingia wastani wa mafungu 9.



Kuna baadhi ya sehemu mafungu hayo wanauza kwa 500 na sehemu nyengine wanauza kwa 1000.



Ukinunua sado moja kwa 3,000 ukauza fungu kwa 500 na ukapanga fungu 9 utapata 4,500. Hapa faida ghafi ni 1,500.



Ukinunua kwa 4,500 ukapanga fungu 7 na kila fungu ukauza kwa 1,000 utapata 7,000. Hapa faida ghafi ni 2,500.



Kwa ufupi katika biashara ya genge katika kila 10,000 unayoingiza faida chache sana utayoipata ni 2,500.



Sasa kazi ni kwako kuangalia sehemu yenye mzunguuko mzuri. Ukiuza bidhaa za 60,000 kwa siku utapata zaidi ya 15,000 faida kwa siku.



Itaendelea.......................................



>>  Endelea kufuatilia makala yetu kila siku.




Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAJI ( MULTI PURPOSE LIQUID SOAP)

*🛑VIFAA MAMA KTK SABUNI YA MAJI*👇🏻ni hivi ndio vinafanya iitwe  sabuni 👇🏻 *Sulphonic acid* *Sless* *Rangi* *Chumvi.* *Manukato* *👉Sulphonic acid* kazi yake kubwa ni kuondoa uchafu wa mahali wakati unatumia sabuni, pia inaongeza uzito na povu ktk sabuni yetu, sulphonic acid ikizidishwa ktk sabuni huleta mchubuko wa mikono kea mtumiaji. *👉Manukato-* kwaajili ya harufu. *👉Sless( ungarol)* Kai yake ni kuleta povu, kuongeza uzito, na pia huondoa uchafu wa mahali wakati unapotumia sabuni. *👉Rangi* Kuleta rangi ya sabuni pekee. *👉Chumvi* Huongeza uzito ktk sabuni, hutunza sabuni isiharibike, pia ikizidishwa hukata sabuni na kuifanya iwe nyepesi Kama maji na kuisha povu. *🛑Hivi ndio👆🏽 vifaa mama ktk utengenezaji was sabuni ya maji* *🛑Vifaa vya nyongeza👇🏻* *📚 Gryselin-* kazi yake kubwa ni kulainisha sabuni na kuzuia michubuko ya ngozi kwa mtumiaji wa sabuni hiyo. *📚 Formaline-* kazi ya yake kutunza sabuni isiharibike, ila formaline ...

JINSI YA KUTENGENEZA HAIR SHAMPOO

 ▶ HAIR SHAMPOO◀ _______________________ Hii ni sabuni ambayo imebuniwa kwa ajili ya kusafishia nywele hata kama zimekaa muda mrefu bila kusafishwa. Hufanya nywele ziwe safi, huondoa uchafu na kuua wadudu walioko kwenye nywele na huondoa mba kwenye nywele. Hapa tutajifunza aina tofauti tofauti za shampoo zikiwemo zenye virutubisho vya matunda na mimea. ▶ SHAMPOO YA NYWELE NZITO NA BORA. 👉MALIGHAFI. 🔸Sless – 1kg. 🔸Cde – 250gm. 🔸Gryceline – vijiko vitano vya chakula (50ml). 🔸Chumvi -500gm. 🔸Rangi – 5gm. 🔸Perfume – 5gm. 🔸Formaline /citric acid – vijiko 3. 🔸Tigna – 125gm. 🔸Maji – 25lt. 👉VIFAA. 🔹Mwiko. 🔹Beseni. 🔹Mask. 🔹Miwani. 🔹Koti. ▶JINSI YA KIUTENGENEZA◀ 1⃣Andaa maji lita 12 kisha tia humo tigna na koroga hadi upate uji mzito kisha weka kando. 2⃣Chukua sless koroga ndani ya maji lita 12 hadi iyeyuke kabisa kisha weka kando. 3⃣Chukua maji nusu lita korogea humo chumvi 500gm hadi iyeyuke yote kisha weka kando.  4⃣Chukua maji robo lita  tia  rangi na korog...

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI Biashara ya kuuza Rasta na Mawigi kwa bei ya jumla, wengi wanapata shida kuja paka Dar kununua Rasta na Mawigi kwa gharama ya juu, mfanyabiashara akiwa mgeni Dar anatumia gharama kubwa sana kwa kufikia Guest pamoja na Chakula. Kama ukiwai kutoa hii huduma kwa wafanyabiashara wa mikoani ni FURSA kwako na unakuwa umewasaidia kupunguza gharama kubwa na kupata faida kuwa kwao. Ukitaka kufanikiwa katika hii biashara fanya yafuatayo : Tafuta maduka yanayouza RASTA & MAWIGI kwa bei ya chini. Ili uweze kutoa OFA nzuri na kupata wateja wengi wa mikoani na kuwasaidia nao kupata faida kubwa kwa kununua kwako. Fungua Instagram Account; post RASTA & MAWIGI aina mbalimbali na bei zake, kumpa mteja njia nyingi za kuchagua bidhaa anayotaka kwenda kuuza kwa wateja wake. Pia post video za watu waliosuka kwa kutumia bidhaa zako au waliotumia kwa kupiga picha. Tumia Bank Account, kupokea malipo kutoka kwa wateja wako; kwa kutumia bank akaunti utakuwa umejilind...