Skip to main content

WAZO LA BIASHARA


                            WAZO LA BIASHARA

IDEA ya Biashara ni moja ya mambo yanayo waumiza watu wengi sana, Na mara nyingi wazo la biashara linahitaji utafiti wa kina ili kuja na wazo lenye tija kwako na kwa jamii nzima.

HIZI NI MOJA YA NJIA ZA KUPATA WAZO LA BIASHARA

1. TUMIA UJUZI ULIO NAO

Ujuzi ulionao ndo sehemu ya kwanza kabisa ya kupata wazo la Biashara, Mfano kama wewe umejiliwa na ni Fundi wa kushona Nguo, why usianze na wewe kuwa na biashara ya aina hiyo? Kama wewe ni fundi magari why usianzishe gereji yako?

Ujuzi ulianao ndo hazina ya kwanza nay a kipekee ya kupata wazo na mara nyingi wajasirimali wengi waliofanikiwa waliacha kazi wanazo fanya na kwenda kuanzisha za aina hiyo na kuzimiliki wenyewe



2. BADILISHA HOBBY YAKO KUWA PESA

Hobby ni moja ya maeneo ambayo watu huja kutajilikia, kama wewe hobby yako ni kufuga mbwa kwa nini usianze hiyo biashara ya kufuga mbwa?

Kama Hobby yako ni Kuogelea, kwa nini usinzishe mabwawa ya kuogelea na wengine wakawa wankuja huko kuogelea?

Kama wewe hobby yako ni upishi kwanini usianzishe mgahawa wako na ukaanza kuuza chakula?

Kam unapenda gardening unaweza anza biashara ya kufanya landscape gardening.



3. NUNUA BIASHARA AMBAYO TIYARI IPO

Ukishindwa kabisa kupa wazo mwanana unaweza nunua biashara ya mtu mwingine na kuindeleza, siku hizu kuna biashara kibao zinauzwa kwa sababu mbalimbali so unaweza nunua nu kuendelea nayo.kwamfano Maduka makubwa ya vyakula, mahoteli, Super market n.k



4. KUNUNUA FRANCHISE

Hii ni moja ya njiza zinazo tumika kwa sasa na sehemu nyingi sana, Unaweza nunua Popular Brand na kuifanyia kazi, Ingawa mara nyingi kuna mashariti ya kuambatana ikiwemo kuhakikisha unatoa huduma sawa na Brandi yenyewe, nah ii ni popular sana katika MAHOTELI/MIGAHAWA, MASUPERMARKET NA MADUKA MENGINE.kwamfano unaweza nunua brand ya kampuni ya Usafirishaji kama vile SUPERFEO na kutoa huduma sawa na wao.

Na usijalibu kutumia Brand ya Kampuni Fulani bila kuwapa Taarifa make inaweza kula kwako na ukajikuta unafilisiwa.

5. TUMIA PERSONALITY YAKO

Kuna watu unakuta either ni Mrembo sana, Handsome na kazalika, unaweza utumia huo urembo na uhendsaamu kufanya biashara, either za marketing,mitindo n.k



6. NINI KINAKOSEKANA MTAANI?

Tazama ni kitu gani hakipo hapo mtaani and then geuza kuwa opportunity, inaweza isiwe ni mtaani ikawa ni kazini kwako, Kijijini kwenum au maeneo unayo enda kustarehe.

-Ni kitu gani huwa kinaleta usumbufu kwako na kukuchukulia muda mwingi na pesa nyingi?

– Ni huduma zipi hazipo kabisa mtaani kwako? Na ambazo ni za muhimu?

-Ni bidhaa zipi ambazo ni vigumu kuzipata mtaani kwenu?

-Ni kitu gani, wewe, Ndugu, Majirini huwa wanakilalamikia sana mtaani hapo?



7. UTALII KATIKA MAENEO YAKO

Hii nayo ni moja ya wazo, so unaweza angalia furusa za utalii kwenye maeneo uliyopo au hata kwingine na kuyafanyia kazi.



8. TUMIA TEKNOLOJIA MPYA KUANZISHA BIASHARA

Angalia mfumo wa maisha wa sasa ulivyo, vitu vinavyo tumika kwa sasa na vinavyo tumiwa na watu wengi, so mfumo wa maisha wa watu kwa sasa unaweza kukuongoza kuja na wazo la Biashara.



9. ANGALIA MAKAMPUNI MAKUBWA NA TAASISI NYINGINE WANAHITAJI NINI?

Unaweza tumia uwepo wa makampuni Fulani au taasisi Fulani maeneo yako kutengeneza wazo la biashara, taasisi kama Shule, vyuo, Hospitali, Makampuni kama Viwanda Migodi na kadhalika, angalia ni kipi hawa watu wanaweza kuwa wanahitaji kwa wingi.



10. UNAWEZA KUANGALIA KUHUSU KUUZA BIDHAA ZA WENGINE

Unaweza ukawa unauza bidhaa za watu wengine, unachukua na kuuza



11. ANGALIA HABARI NA MAKALA MBALIMBALI

Kuna chaneli huwa zina makala mazuri sana ya kiuchumi na biashara, hata TBC huwa ina makala Fulani nzuri sana, na kuna chaneli za kimataifa siku huzi kazi yao ni hiyo tu, ni kuonyesja ubunifu wa wajasirimali, so TV, radio na magazeti yanaweza toa mchango w akutosha kwa wewe kupata wazo la biashara



12. COPY BUSINESS IDEA AMBAYO IMEFANIKIWA KWINGINEKO

Hii ni moja ya njia zinazo tumika kwa sasa, unaweza copy idea kutoka hata India, China, na kwingineko na ukaja kuifanyia kazi huku kwa kufanya marekebisho madogo kulingana na mahitaji ya eneo husika



13. TUMIA NJIA ZOTE ZA KIUTAFITI KUPATA WAZO LA BIASHARA

– Maonyesho ya biashara

– Magazeti,

– Kwenye taasisi za uma zinazo husika na biashara

– Kwa marafiki.



14. UNAWEZA GUNDUA KITU?

Unaweza ukaja na ugunduzi wako kama walivyo fanya wakina Thomas Edson Michael Dell na wengineo, na ikawa ndo mwanzo wa mafanikio kwako.



Kwa maoni zaid toa comment yako hapo chini

Nyamka company ltd

www.nyamkacollection21.blogspot.com








Comments

  1. Kiukweli unatufungua ubongo xaana! Nimeudhuria semina nying za ujasiliamali lkn kwako nimepata v2 vpya kabisa
    🙏shukran

    ReplyDelete

Post a Comment