Skip to main content

NJIA 5 ZA KUPATA WAZO LA BIASHARA


  NJIA 5 ZA KUPATA WAZO LA BIASHARA BORA



1: TAFUTA UHITAJI

Kila mafanikio ni matokeo ya

uhitaji wa watu. Kila unacholi­pia pesa, kwako ni UHITAJI na kwa unayempa pesa ni kuwa AMETATUA TATIZO lako.

Kwa maneno mengine. Kadiri unavyoweza kutatua matatizo MAKUBWA na MENGI ndivyo unavyopata vyanzo vya pesa zaidi. Kwa ufupi umaskini ni matokeo ya kukimbia kutatua matatizo na utajiri ni matokeo ya kukimbilia kutatua matatizo.

Leo ningependa tuangalie njia kadhaa za namna ya kupata mawazo yanayoweza kuwa chanzo cha kubadilisha maisha yako unapoamua kuyafanyia kazi.

Na hapa ningependa kuwa­kumbusha maneno ya William Cameron aliyesema; “Money never starts an idea; it is the idea that starts the money.”

Fedha haileti mawazo ila ma­wazo ndiyo huleta pesa, ndiyo maana kuna watu walishawahi kupata pesa nyingi ila kwa ku­kosa mawazo wamerudi katika kufeli na umaskini.

Hebu chukua dakika moja, jiulize; Katika mazingira niliyopo, je, kuna uhitaji gani ninaoweza kuutatua? Chukua note book yako na andika kabla hatujaen­delea.



Hivyo basi angalia mazingira yanayokuzunguka, je, kuna uhitaji gani? Kama maji yana­toka mara moja kwa wiki mtaani kwenu, ukifanikiwa kununua simtank kadhaa na kuuza maji siku ambazo hayatoki hapo unakuwa umetatua tatizo na umepata pesa. Kama umeg­undua watu karibu na maeneo ya kwenu wanatumia gesi na hakuna duka la karibu, tafuta namna ya kuwa wakala wa kuuza, kadhalika na mahitaji mengine eneo ulilopo.



2: BORESHA WAZO LA MWINGINE

Kuna wakati mwingine hutahita­ji kuanza na wazo jipya kabisa, badala yake utahitaji kuchukua wazo la mwingine kuliboresha. Kwa mfano badala ya mtu kuuza matunda na kuyamenya mtu anaponunua mwingine ak­aboresha akaamua kuyamenya kabisa kisha anayapaki vizuri tayari kwa kuyauza.

Chunguza kile ambacho kina­fanywa na wengine kisha jiulize, hivi nawezaje kuliboresha wazo hili?

3: HAMISHA WAZO LA WENGINE NA LIPE UHALISIA WA MAZINGIRA YAKO

Kuna mawazo mengi yaliyofani­kiwa leo ni matokeo ya mawazo yaliyohamishwa kutoka mahali pengine na yakapewa uhalisia wa mahali husika. X-Factor ya Uingereza imezaa Bongo Star Search, DECA na SONY Records label ndiyo leo tunaona WCB.

Jaribu kuangalia, kuna wazo gani ambalo unaweza kuli­chukua na ukaliwekea mazin­gira ya kwako na ukalifanyia kazi. Unaweza kulitoa nje ya Tanzania na ukalileta Tanzania au ukalitoa Dar na ukalipeleka katika mkoa unaoishi.



4: RAHISISHA MCHAKATO WA KITU AMA BIDHAA FULANI.

Sasa hivi kila mtu anajitahidi kutumia teknolojia kuuza bidhaa au kutoa huduma. Kwa nini? Kwa sababu ya kurahisisha mchakato kwa wateja.Tunaishi katika ulimwengu ambao watu hupenda kutumia muda mfupi kupata huduma au bidhaa, hivyo unachotakiwa kufanya ni kuhak­ikisha kuwa hata kama unatoa bidhaa au huduma ileile kama wengine, jaribu kurahisisha.

Ndiyo maana visimbuzi wanaweka huduma zao kwenye MPESA, Tigopesa, Airtel n.k, wanachojaribu kufanya ni kura­hisisha.

Ni rahisi kwa mama ntilie anayepeleka chakula maofisini na akaongeza gharama ya us­afiri juu ya 500 kwa kila sahani kuliko auze bei ya chini huku ak­isubiri watu wamfuate kilometa moja kule anakouza.



Inawezekana unataka ku­fanya kitu ambacho kila mtu anafanya, swali ni je, unaweza kutoa urahisi gani utakaovutia wanunuaji wa huduma au bid­haa yako?



5: TENGENEZA UHITAJI

Hii si njia rahisi sana ila in­awezekana. Inamaanisha kuna vitu vingi watu wanahitaji ila ha­wawezi kuvitumia hadi viwepo.

Kabla soda hazijaja watu wa­likuwa wanakunywa maji, kabla TV hazipo watu walikuwa ni radio tu na hakuna mtu alikuwa anadai TV kwa kuwa haiku­wepo. Lakini leo ni kama vile haiwezekani kuishi bila TV. Kuna mtu siku moja akauliza; “Hivi wazee wa zamani waliishije bila simu? Miahadi walifanyaje wakifika Kariakoo na kila mtu yuko kona yake?”

Hii ina maana kuna mahitaji mengi bado yako ila watu ha­wawezi kuyadai au kuulizia hadi yatakapokuwepo. Zamani scrub hazikuwepo ukienda saloon, lakini siku hizi ni kama vile ni lazima kila ukinyoa utajikuta unataka kufanya na scrub, tena ina bei kubwa kuliko hata kunyoa kwenyewe!

Hiyo inamaanisha kuna wazo unaweza ukaja nalo watu wakaanza kuhitaji hata kama hawajawahi kujua kama wana­hitaji.



                                    MWISHO

Nyamka comapny ltd

www.nyamkacollection21.blogspot.com














Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAJI ( MULTI PURPOSE LIQUID SOAP)

*🛑VIFAA MAMA KTK SABUNI YA MAJI*👇🏻ni hivi ndio vinafanya iitwe  sabuni 👇🏻 *Sulphonic acid* *Sless* *Rangi* *Chumvi.* *Manukato* *👉Sulphonic acid* kazi yake kubwa ni kuondoa uchafu wa mahali wakati unatumia sabuni, pia inaongeza uzito na povu ktk sabuni yetu, sulphonic acid ikizidishwa ktk sabuni huleta mchubuko wa mikono kea mtumiaji. *👉Manukato-* kwaajili ya harufu. *👉Sless( ungarol)* Kai yake ni kuleta povu, kuongeza uzito, na pia huondoa uchafu wa mahali wakati unapotumia sabuni. *👉Rangi* Kuleta rangi ya sabuni pekee. *👉Chumvi* Huongeza uzito ktk sabuni, hutunza sabuni isiharibike, pia ikizidishwa hukata sabuni na kuifanya iwe nyepesi Kama maji na kuisha povu. *🛑Hivi ndio👆🏽 vifaa mama ktk utengenezaji was sabuni ya maji* *🛑Vifaa vya nyongeza👇🏻* *📚 Gryselin-* kazi yake kubwa ni kulainisha sabuni na kuzuia michubuko ya ngozi kwa mtumiaji wa sabuni hiyo. *📚 Formaline-* kazi ya yake kutunza sabuni isiharibike, ila formaline ...

JINSI YA KUTENGENEZA HAIR SHAMPOO

 ▶ HAIR SHAMPOO◀ _______________________ Hii ni sabuni ambayo imebuniwa kwa ajili ya kusafishia nywele hata kama zimekaa muda mrefu bila kusafishwa. Hufanya nywele ziwe safi, huondoa uchafu na kuua wadudu walioko kwenye nywele na huondoa mba kwenye nywele. Hapa tutajifunza aina tofauti tofauti za shampoo zikiwemo zenye virutubisho vya matunda na mimea. ▶ SHAMPOO YA NYWELE NZITO NA BORA. 👉MALIGHAFI. 🔸Sless – 1kg. 🔸Cde – 250gm. 🔸Gryceline – vijiko vitano vya chakula (50ml). 🔸Chumvi -500gm. 🔸Rangi – 5gm. 🔸Perfume – 5gm. 🔸Formaline /citric acid – vijiko 3. 🔸Tigna – 125gm. 🔸Maji – 25lt. 👉VIFAA. 🔹Mwiko. 🔹Beseni. 🔹Mask. 🔹Miwani. 🔹Koti. ▶JINSI YA KIUTENGENEZA◀ 1⃣Andaa maji lita 12 kisha tia humo tigna na koroga hadi upate uji mzito kisha weka kando. 2⃣Chukua sless koroga ndani ya maji lita 12 hadi iyeyuke kabisa kisha weka kando. 3⃣Chukua maji nusu lita korogea humo chumvi 500gm hadi iyeyuke yote kisha weka kando.  4⃣Chukua maji robo lita  tia  rangi na korog...

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI Biashara ya kuuza Rasta na Mawigi kwa bei ya jumla, wengi wanapata shida kuja paka Dar kununua Rasta na Mawigi kwa gharama ya juu, mfanyabiashara akiwa mgeni Dar anatumia gharama kubwa sana kwa kufikia Guest pamoja na Chakula. Kama ukiwai kutoa hii huduma kwa wafanyabiashara wa mikoani ni FURSA kwako na unakuwa umewasaidia kupunguza gharama kubwa na kupata faida kuwa kwao. Ukitaka kufanikiwa katika hii biashara fanya yafuatayo : Tafuta maduka yanayouza RASTA & MAWIGI kwa bei ya chini. Ili uweze kutoa OFA nzuri na kupata wateja wengi wa mikoani na kuwasaidia nao kupata faida kubwa kwa kununua kwako. Fungua Instagram Account; post RASTA & MAWIGI aina mbalimbali na bei zake, kumpa mteja njia nyingi za kuchagua bidhaa anayotaka kwenda kuuza kwa wateja wake. Pia post video za watu waliosuka kwa kutumia bidhaa zako au waliotumia kwa kupiga picha. Tumia Bank Account, kupokea malipo kutoka kwa wateja wako; kwa kutumia bank akaunti utakuwa umejilind...