Skip to main content

MAMBO 5 YA KUFANYA KWENYE MTANDAO KUWAFIKIA WATU WENGI NA KUUZA BIDHAA NYINGI


Mambo 5 Ya Kufanya Kwenye Mtandao Kuwafikia Watu Wengi Na Kuuza Bidhaa Nyingi.



Kama wewe ni mjasiriamali mwenye bidhaa au huduma nzuri lakini unashindwa kuwafikia watu wengi kwenye mtandao basi hakikisha unanipa macho na masikio yako kwani huenda makala hii ikawa moja ya makala muhimu utakayosoma mwaka huu.



Kutokana na uzoefu wetu wa kutumia mtandao kwa miaka zaidi ya 6 kupata wateja, tumegundua kuna mambo 5 ukiyafanya vizuri basi utawafikia watu wengi na kuuza bidhaa nyingi sana.



Mambo yenyewe ni:



1. Zingatia Ubora:

Zingatia ubora

Ukiwa unatoa bidhaa au huduma nzuri kwenye soko yenye kutatua matatizo ya wateja wako, basi utapata majeshi ya watu watakaokusaidia kusambaza ujumbe kuhusu bidhaa yako bila ya wewe kuwalipa chochote.



Wajasiriamali wa Silicon Valley, Marekani wana msemo wao unaosema,



The goal is to develop a product so good that customers will move the products for us before we consider marketing it.



Yaani,



Lengo ni kutengeneza bidhaa nzuri sana kiasi ambacho wateja wetu watatutangazia kwenye soko kabla ya sisi kufikiria kuitangaza wenyewe.



Na moja kati ya sifa muhimu wawekezaji wa makumpuni ya Silicon Valley (akina Facebook) wanaangali ni bidhaa nzuri zinazoweza kutangazwa na watumiaji!



2. Kuwa Tofauti

Kuwa Tofauti - Jinsi Ya Kutumia Mtandao Kuwafikiwa Watu Wengi

Ukiwa tofauti unakumbukwa.



Moja ya kosa kubwa linalofanywa na wafanyabiashara wengi ni kuangalia washindani wako wanafanya nini na kuwaiga.



Ukifanya hivyo basi usitegemee biashara yako kudumu miaka mingi.



Kuwa mbunifu na jiweke tofauti kabisa na washindani wako.



Mfano mzuri ni kampuni ya viatu iitwayo Vibram Five fingers, viatu vilivyokaa kama glovu za mikono.



Vibram 5 Fingers - Viatu kama gloves

Walipoviingiza viatu vyao sokoni vilianza kuenea kama virusi vya flu na kila aliyekuwa anaviona viatu hivyo alikuwa akivitamani.



Kwa nini? Mbali na bidhaa yao kuwa nzuri, walikuwa tofauti kabisa na viatu vyengine.



Ukiwa tofauti utakumbukwa siku zote.



Hutafananishwa na mamia ya washindani wako wanaofanana.



Na kila ikiwa rahisi kukumbukwa inakuwa ni rahisi vile vile kuwafikia watu wengi.



3. Toa Kabla Hujapokea

Toa kabla hujapokea - Jinsi ya kutumia mtandao kuwafikia wateja wengi

Japokuwa umeanzisha biashara yako kutengeneza pesa, jiulize kitu gani unaweza kutoa BURE kabla ya kuuza bidhaa yoyote?



Hii ni muhimu sana kwani wateja wako watarajiwa hawakujui, hawakupendi na wala hawakuamini.



Kwa hivyo ukiwazawadia kitu chochote, utajenga uaminifu kwa urahisi na kwa kasi kubwa sana hususani katika mtandao.



Vitu unavyoweza kutoa ni kama:



Ushauri

Sampuli ya bidhaa

Mafunzo (kama haya tunayookupa sisi)

N.k. (Kuwa mbunifu)



Lengo la utoaji ni kuwaonesha wateja wako watarajiwa kuwa haupo pale kula pesa zao bali unawajali na unataka bidhaa / huduma unayotoa iwasaidie kutatua matatizo yao.



4. Tengeneza Smaku Ya Kunasa Wateja Kwenye Mtandao

Nasa wateja kama smaku

Tengeneza mashine kwenye mtandao yenye kuwasiliana na wateja wako watarajiwa, kukujengea uaminifu na kukuuzia bidhaa zako kwa niaba yako.



5. Tangaza! Tangaza! Tangaza!

tangaza. Jambo la tano na la muhimu sana la kufanya kuweza kuwafikia watu na kuuza bidhaa nyingi ni kutangaza.



Matangazo ni kama petroli kwenye gari lako.



Ukiacha kutangaza biashara yako haisogei mbele. Inakwama au inarudi nyuma.



Kwa vile washindani wamekuwa wengi kutangaza si jambo la hiari.



Ila ni muhimu kuzingatia matunda unayopata kutokana na kila tangazo uweze kuboresha na yazidi kukuletea faida.



Lengo ni kuwekeza pesa yenye kukusaidia kuleta mauzo yenye faida kubwa kuliko gharama za matangazo yako na kuendelea kufanya hivyo kila siku ili biashara yako ikuwe.



Ukiwa na mfumo mzuri kwenye biashara yako (ya mtandaoni na nje ya mtandao) kazi yako kubwa itakuwa ni

Kutangaza na

Kuboresha bidhaa na huduma zako

Natumai umefaidika na makala hii.



Tujulishe kwa ku comment hapo chini, njia zipi unazotumia kwenye mtandao kuwafikia wateja wako.

Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAJI ( MULTI PURPOSE LIQUID SOAP)

*🛑VIFAA MAMA KTK SABUNI YA MAJI*👇🏻ni hivi ndio vinafanya iitwe  sabuni 👇🏻 *Sulphonic acid* *Sless* *Rangi* *Chumvi.* *Manukato* *👉Sulphonic acid* kazi yake kubwa ni kuondoa uchafu wa mahali wakati unatumia sabuni, pia inaongeza uzito na povu ktk sabuni yetu, sulphonic acid ikizidishwa ktk sabuni huleta mchubuko wa mikono kea mtumiaji. *👉Manukato-* kwaajili ya harufu. *👉Sless( ungarol)* Kai yake ni kuleta povu, kuongeza uzito, na pia huondoa uchafu wa mahali wakati unapotumia sabuni. *👉Rangi* Kuleta rangi ya sabuni pekee. *👉Chumvi* Huongeza uzito ktk sabuni, hutunza sabuni isiharibike, pia ikizidishwa hukata sabuni na kuifanya iwe nyepesi Kama maji na kuisha povu. *🛑Hivi ndio👆🏽 vifaa mama ktk utengenezaji was sabuni ya maji* *🛑Vifaa vya nyongeza👇🏻* *📚 Gryselin-* kazi yake kubwa ni kulainisha sabuni na kuzuia michubuko ya ngozi kwa mtumiaji wa sabuni hiyo. *📚 Formaline-* kazi ya yake kutunza sabuni isiharibike, ila formaline ...

JINSI YA KUTENGENEZA HAIR SHAMPOO

 ▶ HAIR SHAMPOO◀ _______________________ Hii ni sabuni ambayo imebuniwa kwa ajili ya kusafishia nywele hata kama zimekaa muda mrefu bila kusafishwa. Hufanya nywele ziwe safi, huondoa uchafu na kuua wadudu walioko kwenye nywele na huondoa mba kwenye nywele. Hapa tutajifunza aina tofauti tofauti za shampoo zikiwemo zenye virutubisho vya matunda na mimea. ▶ SHAMPOO YA NYWELE NZITO NA BORA. 👉MALIGHAFI. 🔸Sless – 1kg. 🔸Cde – 250gm. 🔸Gryceline – vijiko vitano vya chakula (50ml). 🔸Chumvi -500gm. 🔸Rangi – 5gm. 🔸Perfume – 5gm. 🔸Formaline /citric acid – vijiko 3. 🔸Tigna – 125gm. 🔸Maji – 25lt. 👉VIFAA. 🔹Mwiko. 🔹Beseni. 🔹Mask. 🔹Miwani. 🔹Koti. ▶JINSI YA KIUTENGENEZA◀ 1⃣Andaa maji lita 12 kisha tia humo tigna na koroga hadi upate uji mzito kisha weka kando. 2⃣Chukua sless koroga ndani ya maji lita 12 hadi iyeyuke kabisa kisha weka kando. 3⃣Chukua maji nusu lita korogea humo chumvi 500gm hadi iyeyuke yote kisha weka kando.  4⃣Chukua maji robo lita  tia  rangi na korog...

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAGADI/KIGOMA/GWANJI

Jinsi ya kutengeneza Sabuni ya magadi( gwanji)ama Sabuni ya kigoma. MAHITAJI Caustic Soda kilo 3 Mafuta ya mawese lita 20 Sodium Silicate Maji lita 10 Rangi ya bluu vijiko 3 Jinsi ya kutengeneza. 1)Chukuwa coustic soda changanya na maji na uanze kukoroga kuelekea upande mmoja endelea kufanya hivyo hadi vichanganyikane vizur baada ya hapo iache kwa saa 24 2)Chukuwa kindoo kidogo na upunguze mafuta lita 3 kwa ajili ya kuweka rangi pembeni,weka rangi vijiko 3 ,changanya na mafuta uliyopunguza lita 3 kisha koroga mpaka yachanganyikane vizur kabisa 3)Chukuwa coustic soda uliyoloweka kwenye ndoo kubwa ,kisha tia mafuta na uendelee kukoroga kuekekea upande mmoja kwa nguvu na kwa haraka,tia sodium silgett kwa kunyunyuzia kidogo kidogo, endelea kukoroga hadi vichanganyikane viwe kitu kimoja 4)Baada ya hapo andaa ndoo nyingine ndogo ,chukuwa uji uliokoroga au mkorogo wako kias kwa ajili ya kuchanganya na rangi mwanzo na mafuta kisha koroga kwa pamoja vichanganyikane vizur ...