Skip to main content

BIASHARA YA STATIONARY


           BIASHARA YA STATIONARY

Biashara ya stationary imekuwa maarufu sana tanzania nzima, wanaofanya wengi wanajua vitu ambavyo wengi wanajua ndo maana wanagawana wateja na baadhi ya waanzilishi wanashindwa na kufunga ofisi.

Wengi wanafanya biashara hii kwa mazoea na sio kwa ubunifu na mwendelezo wa kujifunza zaidi na zaidi na kuwa bora kwenye kazi yake.

Wengi hawajui kubuni kazi mpya zinazotokana na printing, wengi wanatumia PUBLISHER kutengeneza kadi n.k bila kujua kuna kitu kinaitwa ADOBE ILLUSTRATOR, ADOBE PHOTOSHOP, ADOBE FIREWORKS n.k ambazo ukitumia hizo software unatengeneza kadi ambazo utakuwa tofauti kabsa na wengine , ila watu wanapenda vitu virahisi ndo maana hatuon faida kwenye stationary baadae kufunga ofisi na kutafuta biashara zingine.



Kama unataka kufanikiwa kwenye biashara ya stationary fuata hatua zifuatazo bila kuruka:



1. Penda kujifunza zaidi kuhusu huduma zitokanazo na printing. Usipenda rahisi kutoka publisher wengi wanafanya na kufanya wateja wasione utofauti na kwenda stationary ile wanayoiona mbele yao.



2. Kuwa mbunifu. Buni kitu ambacho kitakitofautisha na wengine na kuwe kwenye category mpya ambayo sokoni haipo. Google Google Google ni dizan gani mpya ya kutengeneza kadi kwa sasa.



3. Jifunze kununua vitu online na sio tz. Fanya jitihada yoyote kujua namna ya kununua vitu online ili uwe na sample ambazo wengine hawana. Kuna notebook niona ebay balaa sidhan kama tz vipo.



4. Location: hii ndo kitu sehem muhimu sana kama hizo step za juu umezifuata bila kuruka, tafuta sehemu ambayo ni karibu na chuo kikuu au ofisi za serikali kama manispaa au tra n.k . Hizo sehemu stationary utaipenda au kutafuta sehemu center(katikati ya mji).



5. Usipenda kufanya kazi pekeyako. Tafuta msaidizi au mtaalamu wa ADOBE ili uwe tofauti kwenye dizani kama kadi, vipeperushi .



6. Tengeneza sample zitokanazo na printing weka sehemu inayoonekana ili wateja waoni. Kumbuka wateja hawajui wanachokitaka paka waoneshe, waoneshe uwezo wako kwa vitendo kuwa mtu wa kuwatamanisha vitu vizuri ambavyo unaviona kwa wazungu na sio kwa wabongo.



7. Weka INTERNET kwenye ofisi yako. Hii itawavuta wateja wanaoweka mavitu yao kwenye email na kutaka kuprint iwe rahisi kwao. Hakikisha internet ipo muda wote.



8. Uza vikorokoro kama PROTECTOR, EARPHONE, COVER, FLASH.



9. Uza na movie za kudownload ili kuwavuta zaidi wateja , fanya mpango uwe na cumputer 2 moja ya mambo ya stationary na nyingine ya kudownload movie , hii ya movie weka UBUNTU kuzuia virus.



10. Computer yenye UBUNTU(Windows). Hii ndio computer ambayo mtu akija na kazi yake kwenye flash , ingiza kwanza kwenye ubuntu na kuangalia kama ina virus ili uwatoe na kulinda computer yako ya WINDOWS 10/8/7 isihasirike na virus.



11. Nenda kwa kujiamini maofisin kuomba tenda za kuprint na ku supply rim. Nenda ukiwa umevaa vizuri na kuonekana smart.



Usisahau kushake mkono na mkuu husika wa kitengo hicho na kumkazia macho usoni na kusema “taja jina lako mwisho sema na furaha ya kuonana na wewe”.



Nilijaribu hivyo nilipoenda manispaa flan mjini hapa kwenye meeting ya kutengeneza SOFTWARE. Kumbuka “Confidence talking produce Confidence thinking”. It work for me…



12. INSTAGRAM ACCOUNT ni lazima

“Ukitaka kufanikiwa haraka, ongeza spidi ya kufeli”




Comments

Popular posts from this blog

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAJI ( MULTI PURPOSE LIQUID SOAP)

*🛑VIFAA MAMA KTK SABUNI YA MAJI*👇🏻ni hivi ndio vinafanya iitwe  sabuni 👇🏻 *Sulphonic acid* *Sless* *Rangi* *Chumvi.* *Manukato* *👉Sulphonic acid* kazi yake kubwa ni kuondoa uchafu wa mahali wakati unatumia sabuni, pia inaongeza uzito na povu ktk sabuni yetu, sulphonic acid ikizidishwa ktk sabuni huleta mchubuko wa mikono kea mtumiaji. *👉Manukato-* kwaajili ya harufu. *👉Sless( ungarol)* Kai yake ni kuleta povu, kuongeza uzito, na pia huondoa uchafu wa mahali wakati unapotumia sabuni. *👉Rangi* Kuleta rangi ya sabuni pekee. *👉Chumvi* Huongeza uzito ktk sabuni, hutunza sabuni isiharibike, pia ikizidishwa hukata sabuni na kuifanya iwe nyepesi Kama maji na kuisha povu. *🛑Hivi ndio👆🏽 vifaa mama ktk utengenezaji was sabuni ya maji* *🛑Vifaa vya nyongeza👇🏻* *📚 Gryselin-* kazi yake kubwa ni kulainisha sabuni na kuzuia michubuko ya ngozi kwa mtumiaji wa sabuni hiyo. *📚 Formaline-* kazi ya yake kutunza sabuni isiharibike, ila formaline ...

JINSI YA KUTENGENEZA HAIR SHAMPOO

 ▶ HAIR SHAMPOO◀ _______________________ Hii ni sabuni ambayo imebuniwa kwa ajili ya kusafishia nywele hata kama zimekaa muda mrefu bila kusafishwa. Hufanya nywele ziwe safi, huondoa uchafu na kuua wadudu walioko kwenye nywele na huondoa mba kwenye nywele. Hapa tutajifunza aina tofauti tofauti za shampoo zikiwemo zenye virutubisho vya matunda na mimea. ▶ SHAMPOO YA NYWELE NZITO NA BORA. 👉MALIGHAFI. 🔸Sless – 1kg. 🔸Cde – 250gm. 🔸Gryceline – vijiko vitano vya chakula (50ml). 🔸Chumvi -500gm. 🔸Rangi – 5gm. 🔸Perfume – 5gm. 🔸Formaline /citric acid – vijiko 3. 🔸Tigna – 125gm. 🔸Maji – 25lt. 👉VIFAA. 🔹Mwiko. 🔹Beseni. 🔹Mask. 🔹Miwani. 🔹Koti. ▶JINSI YA KIUTENGENEZA◀ 1⃣Andaa maji lita 12 kisha tia humo tigna na koroga hadi upate uji mzito kisha weka kando. 2⃣Chukua sless koroga ndani ya maji lita 12 hadi iyeyuke kabisa kisha weka kando. 3⃣Chukua maji nusu lita korogea humo chumvi 500gm hadi iyeyuke yote kisha weka kando.  4⃣Chukua maji robo lita  tia  rangi na korog...

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI Biashara ya kuuza Rasta na Mawigi kwa bei ya jumla, wengi wanapata shida kuja paka Dar kununua Rasta na Mawigi kwa gharama ya juu, mfanyabiashara akiwa mgeni Dar anatumia gharama kubwa sana kwa kufikia Guest pamoja na Chakula. Kama ukiwai kutoa hii huduma kwa wafanyabiashara wa mikoani ni FURSA kwako na unakuwa umewasaidia kupunguza gharama kubwa na kupata faida kuwa kwao. Ukitaka kufanikiwa katika hii biashara fanya yafuatayo : Tafuta maduka yanayouza RASTA & MAWIGI kwa bei ya chini. Ili uweze kutoa OFA nzuri na kupata wateja wengi wa mikoani na kuwasaidia nao kupata faida kubwa kwa kununua kwako. Fungua Instagram Account; post RASTA & MAWIGI aina mbalimbali na bei zake, kumpa mteja njia nyingi za kuchagua bidhaa anayotaka kwenda kuuza kwa wateja wake. Pia post video za watu waliosuka kwa kutumia bidhaa zako au waliotumia kwa kupiga picha. Tumia Bank Account, kupokea malipo kutoka kwa wateja wako; kwa kutumia bank akaunti utakuwa umejilind...