Skip to main content

BIASHARA YA SALOON YA KIUME


                  BIASHARA YA SALOON YA KIUME

Biashara ya saloon ni biashara ya kawaida sana kama utachukulia kimatazamo wa kawaida ila kama utachukulia kwa mtazamo wa kutaka kifika mbali na kubadilisha maisha ni biashara yenye pesa sana kama utakuwa mbunifu kwa kutumia technologia ya sasa.

Kuna msemo unasema kwamba “ukitaka kufanikiwa kwenye biashara yoyote kwa sasa ibadilishe iwe biashara ya kutumia mitandao ya kijamii(social media)”. Sijawai kuona mtu anatangaza biashara yake ya saloon kwenye mitandao ya kijamii kwa kuwa anamini ni biashara ya kawaida sana na haiwezi kumuingizia pesa nyingi ata akitangaza kwenye mitandao ya kijamii. Thana potofu…

Ukitaka kufanikiwa kwenye biashara ya saloon ya kiume fanya yafuatayo bila kuruka hatua ata moja:

  • Tafuta sehemu ambayo ipo maeneo ya barabarani au yenye mkusanyiko mkubwa wa watu. Usiogope kukuta saloon zingine zipo wewe fungua kwa kuwa mbinu unayoenda kuitumia lazima wapinzani wako waombe pooo.
  • Fungua akaunti ya facebook page na instagram , tangaza saloon yako ili watu waone huduma yako ili waje.
  • Anzisha huduma ya malipo ya kabla, mfano kunyoa na kuoshwa ni sh 3000, madharani mtu ananyoa mara 4 kwa mwezi(4×3000 = 12000), wewe weka kunyoa mara 4 kwa mwezi ni sh 10,000; mteja ananyoa kila wiki ndani ya mwezi mzima(ndevu na nywele).  Swala hili litangaze mara nyingi kwenye mitandao ya kijamii uku ukilenga mtaa ofisi ilipo( tabata segerea BIMA) ili matangazo yako yaonekana kwa watu wa mtaani kwako tu ofisi ilipo. Kwa wanataka kulipia kila anaponyoa ni sh 3000.
  • Anzisha huduma ya ushirika wa kuuza huduma, mteja akileta rafiki yake anayoa nusu bei(1500).  Hakikisha huduma yako ni ile ile kwa kila mteja usioneshe upendeleo wa kihuduma kwasababu pesa ni nusu bei ya kunyoa.
  • Weka tv na uwe na movie mpya mpya kwenye flash ili mteja asiboreke kipindi anasubiria huduma. Hakikisha movie ni HD na sizisho tasiriwa kiswahili.
  • Kuwa mtu wa stori nyingi zenye kujenga hoja kipindi unatoa huduma usinyamaze kama bubu. Penda kutumia FOCUS QUESTIONS , ku challenge mindset za wateja wako.
  • Hakikisha vitaulo ni visafi muda wote na kutumia heater kuchoma machine zako mbele ya mteja. Kufanya hivyo mbele ya mteja inaonesha unajali afya yake.
  • Penda kuuliza kama mtu anapenda kuchonga au laah, vinyozi wengine wameshakalilia kila mteja anachonga bila kuliza na kuonekana anafanya kazi kwa mazoea. Usifanye hivyo wateja wengi hawapendi even mm sipendi..
  • Penda kushukuru mteja anapotoa pesa na kukulipa, ni haki yako lakini wewe shukuru mzee baba.
  • Post video instagram na facebook post picha kila siku saa 11 jion ukiwa unanyoa saloon.  Penda kuliza mswali kujua mawazo ya wateja wako instagram na facebook. Penda sana kujua mapendekezo ya wateja wako ni yapi , wapi uboreshe ili wateja wapenda sana huduma yako na kuvuta marafiki zao kuja kwako.
  • Penda kutoa ofa kila wiki kwa wateja ambao hawapo kwenye malipo ya kabla, kila wiki end au mwisho wa mwezi nyoa kwa nusu bei kama kurudisha fadhila kwa wateja wako ili hudumu nao kwenye biashara yako(Wateja wanapenda marejesho yenye faida)
  • Penda kuvaa mavazi yanayoonesha unajali afya yako , swali unawezaje kujali afya ya mwingine wakati wewe yako umeshindwa,  kwa lugha ya kwenye ndege wanasemaga “Vaa mask ya oxygen kwanza wewe kabla ujamvalisha mwingine”.
  • Kuwa msafi muda wote kwa gharama yoyote maana ndiyo sifa pekee itakayo kufanya wateja waje kwako kwa muonekano wako kila siku. Mfano unayolewaje na mtu ananuka kwapa au anajikuna muda mwingi au mmbwa zimemjaa mwili wote paka anatisa kumwangalia. Mswaki kwako uwe kipaumbele..
  • Saloon iwe safi muda wote , epuka manywel kuzaga zaga ovyo kwenye floor inatia kinyaa kwa mteja kukaa na kunyolewa. Pia yale mapazia ya kufunikiwa wateja wasitapakae nywele nayo yawe mengi kidogo na masafi kila siku.
  • Fikiria kuhusu generator siku za usoni , ili mteja awe na uwakika wa kupata huduma hata kama umeme ukikatika.

“The most successful businesses today (big or small) are those that see themselves as “technology” companies, irrespective of what business they are in!”










Comments

  1. ushaur mzuri sana nami nataka nianishe karibuni naomben ushauri wenu zaidi

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

JINSI YA KUTENGENEZA SABUNI YA MAJI ( MULTI PURPOSE LIQUID SOAP)

*🛑VIFAA MAMA KTK SABUNI YA MAJI*👇🏻ni hivi ndio vinafanya iitwe  sabuni 👇🏻 *Sulphonic acid* *Sless* *Rangi* *Chumvi.* *Manukato* *👉Sulphonic acid* kazi yake kubwa ni kuondoa uchafu wa mahali wakati unatumia sabuni, pia inaongeza uzito na povu ktk sabuni yetu, sulphonic acid ikizidishwa ktk sabuni huleta mchubuko wa mikono kea mtumiaji. *👉Manukato-* kwaajili ya harufu. *👉Sless( ungarol)* Kai yake ni kuleta povu, kuongeza uzito, na pia huondoa uchafu wa mahali wakati unapotumia sabuni. *👉Rangi* Kuleta rangi ya sabuni pekee. *👉Chumvi* Huongeza uzito ktk sabuni, hutunza sabuni isiharibike, pia ikizidishwa hukata sabuni na kuifanya iwe nyepesi Kama maji na kuisha povu. *🛑Hivi ndio👆🏽 vifaa mama ktk utengenezaji was sabuni ya maji* *🛑Vifaa vya nyongeza👇🏻* *📚 Gryselin-* kazi yake kubwa ni kulainisha sabuni na kuzuia michubuko ya ngozi kwa mtumiaji wa sabuni hiyo. *📚 Formaline-* kazi ya yake kutunza sabuni isiharibike, ila formaline ...

JINSI YA KUTENGENEZA HAIR SHAMPOO

 ▶ HAIR SHAMPOO◀ _______________________ Hii ni sabuni ambayo imebuniwa kwa ajili ya kusafishia nywele hata kama zimekaa muda mrefu bila kusafishwa. Hufanya nywele ziwe safi, huondoa uchafu na kuua wadudu walioko kwenye nywele na huondoa mba kwenye nywele. Hapa tutajifunza aina tofauti tofauti za shampoo zikiwemo zenye virutubisho vya matunda na mimea. ▶ SHAMPOO YA NYWELE NZITO NA BORA. 👉MALIGHAFI. 🔸Sless – 1kg. 🔸Cde – 250gm. 🔸Gryceline – vijiko vitano vya chakula (50ml). 🔸Chumvi -500gm. 🔸Rangi – 5gm. 🔸Perfume – 5gm. 🔸Formaline /citric acid – vijiko 3. 🔸Tigna – 125gm. 🔸Maji – 25lt. 👉VIFAA. 🔹Mwiko. 🔹Beseni. 🔹Mask. 🔹Miwani. 🔹Koti. ▶JINSI YA KIUTENGENEZA◀ 1⃣Andaa maji lita 12 kisha tia humo tigna na koroga hadi upate uji mzito kisha weka kando. 2⃣Chukua sless koroga ndani ya maji lita 12 hadi iyeyuke kabisa kisha weka kando. 3⃣Chukua maji nusu lita korogea humo chumvi 500gm hadi iyeyuke yote kisha weka kando.  4⃣Chukua maji robo lita  tia  rangi na korog...

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI

BIASHARA YA KUUZA RASTA NA MAWIGI Biashara ya kuuza Rasta na Mawigi kwa bei ya jumla, wengi wanapata shida kuja paka Dar kununua Rasta na Mawigi kwa gharama ya juu, mfanyabiashara akiwa mgeni Dar anatumia gharama kubwa sana kwa kufikia Guest pamoja na Chakula. Kama ukiwai kutoa hii huduma kwa wafanyabiashara wa mikoani ni FURSA kwako na unakuwa umewasaidia kupunguza gharama kubwa na kupata faida kuwa kwao. Ukitaka kufanikiwa katika hii biashara fanya yafuatayo : Tafuta maduka yanayouza RASTA & MAWIGI kwa bei ya chini. Ili uweze kutoa OFA nzuri na kupata wateja wengi wa mikoani na kuwasaidia nao kupata faida kubwa kwa kununua kwako. Fungua Instagram Account; post RASTA & MAWIGI aina mbalimbali na bei zake, kumpa mteja njia nyingi za kuchagua bidhaa anayotaka kwenda kuuza kwa wateja wake. Pia post video za watu waliosuka kwa kutumia bidhaa zako au waliotumia kwa kupiga picha. Tumia Bank Account, kupokea malipo kutoka kwa wateja wako; kwa kutumia bank akaunti utakuwa umejilind...